University of Kabianga Repository

Changamoto Zinazokabili Umiliki na Matumizi ya Ardhi Barani Afrika: Udurusu wa Riwaya Tatu za Karne ya 21

Show simple item record

dc.contributor.author Muhia, Arthur K.
dc.contributor.author Mwamzandi, Issa Y.
dc.date.accessioned 2024-03-05T08:04:55Z
dc.date.available 2024-03-05T08:04:55Z
dc.date.issued 2022
dc.identifier.citation Muhia, A. K., & Mwamzandi, I. Y. (2022). Changamoto Zinazokabili Umiliki na Matumizi ya Ardhi Barani Afrika: Udurusu wa Riwaya Tatu za Karne ya 21. Mwanga wa Lugha, 7(1), 77-88. en_US
dc.identifier.uri http://ir-library.kabianga.ac.ke/handle/123456789/775
dc.description Jarida la Changamoto Zinazokabili Umiliki na Matumizi ya Ardhi Barani Afrika: Udurusu wa Riwaya Tatu za Karne ya 21 en_US
dc.description.abstract Makala haya yanachanganua suala la changamoto zinazokabili umiliki na matumizi ya ardhi barani Afrika kama lilivyosawiriwa katika riwaya za karne ya ishirini na moja, kwa kurejelea riwaya za Chozi la Heri (2014), Msimu wa Vipepeo (2009) na Nakuruto (2006). Ardhi ni miongoni mwa rasilimali muhimu katika maisha ya binadamu hasa katika uzalishaji mali. Huwa chanzo cha mahitaji ya kimsingi kama vile chakula na makaazi. Aidha, uwezo wa kumiliki ardhi huwa ni sifa kuu ya maendeleo na mabadiliko mengi katika jamii ambayo yamewahi kushuhudiwa duniani. Tungo za kifasihi tulizoziteua kimakusudi zilifanikisha utafiti huu kwa sababu fasihi huwa imefungamanishwa kibunifu na maisha halisi ya binadamu. Sifa kuu ya riwaya hizi ni kwamba zimeliangazia suala la ardhi kwa mapana. Isitoshe, zimetungwa katika kipindi cha karne ya ishirini na moja ambacho utandawazi umeenea na kuimarika barani Afrika. Ili kufanikisha udurusu huu, tuliligawa suala letu la utafiti katika sehemu tatu kuu: kipindi cha kabla ya ukoloni, kipindi cha ukoloni na kipindi cha utandawazi. Uchanganuzi matini huu wa kimaktaba uliongozwa na nadharia ya Baada-ukoloni. Umuhimu wa makala haya unatarajiwa kuwa pamoja na kudhihirisha mitazamo ya watunzi mbalimbali kuhusu changamoto katika umiliki na matumizi ya ardhi barani Afrika; pamoja na mapendekezo ya namna za kuzitatua. Tunatarajia kutoa mchango wa kitaaluma kuhusiana na suala hili hivyo kuwafaa watafiti wa baadaye na watunga sera zinazohusiana na suala la umiliki na matumizi ya ardhi barani Afrika. en_US
dc.language.iso other en_US
dc.publisher Mwanga wa Lugha, 7(1), 77-88. en_US
dc.subject Ardhi en_US
dc.subject Utandawazi en_US
dc.title Changamoto Zinazokabili Umiliki na Matumizi ya Ardhi Barani Afrika: Udurusu wa Riwaya Tatu za Karne ya 21 en_US
dc.type Article en_US


Files in this item

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search DSpace


Browse

My Account