Kutumiya Alama za Kifasihi Kisiyasa ili Kušajiiša Mṭaji wa Kijamii: Kaďiya ya Sufi Ṁanalemba Kuvunja Upanga katika Uṭeṇḍi wa Siri Li Asrari

Loading...
Thumbnail Image

Date

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

East African Journal of Swahili Studies

Abstract

Fasiri nyengine za kazi za kifasihi zapatikana k̇ a kutiliya maanani mukṭaďa wa kihistoriya wa kazi hiyo. Fauka ya hayo, iṭikaḍiza kisiyasa, kiḍini, au kijinsiya ni miyongoni ṁa paradimu zinazoongoza muwonouliṁengu wa mtunzi wa kazi za kisanaa. Katika mfanyiko huu wa kučanganya masiyala ya kijamii na ya kiimani nripo uṭafiṭi wetu ulipoďamiriya kuuhakiki Uṭeṇḍi wa Siri li Asrari uliyotunġa ni Ṁanaṁarabu binṭi ḂanaLemba mnamo 1662 huko Paṭe, Kenya. Makala yetu yamejaribu kujibu maswali: mukṭaďa wa kihistoriya wa wakaṭi na mahali ulimšajiišaje mtunzi kuwasiliša ďamira yake k̇ a mbinu ya kinahau? Je, ḍini, haswa ďehebu la kiSufi, iličangiyaje muwonouliṁengu wa mtunzi wakaṭi wa kuwasiliša alama za kiḍini katika kazi hiyo? Je, suluhišo la mtunzi kuhusu mukṭaďa wa siyasa ya wakaṭi huwo k̇ a mkonro wa imani yake ulitatuwaje maafa ya wakaṭi huwo? Tuličanganuwa maṭini ya uṭeṇḍi huu tukiyongozwa ni naďariya ya uHistoriya Mpya k̇ a k̇ angaziya: alama, jazanra, ṭaswira, siṭiyara, kiyasi zilivotumiwa na mtunzi na aťari zake katika mfanyiko mzima wa kisiyasa. Data ya upili ilikusanywa ili tupate fasiri nyenginezo kuṭokana na mukṭaďa huwo k̇ a sababu hayakujiṭokeza mayelezo haya katika uṭeṇḍi. Maṭokeyo yetu yanaďihiriša: k̇ a kučanganuliwa luǧa ya nje kiyasi ya vita va Mtume Muhammaḍ (mhusika nguli) na Anďaruni (mhusika nruli) ilikuwa ni siṭiyara ya matukiyo ya wakaṭi huwo. Hali kaďalika, mtunzi ališajiišwa ni matukiyo hayo k̇ enye uwasilišaji wake ambawo ulifasiri nahau za kusikiya siyasa (hisiya zake za mukṭaďa wa wakaṭi, mahali, na hali), k̇ ingiliya siyasa (kuyazungumziya matukiyo), na kuleta siyasa (kukosowa kupita mipaka)—unukuďi wa msimamo wa aila yake ambao ni sosiyasa (maSufi hawaingii siyasani). Kinyumeče, data ilipočanganuliwa k̇ a minaṭarafu ya luǧa ya nrani ya kifasihi ya kiSufi iliďihirika maana ya nahau kutumiya siyasa ni kutumiya hekima kuwaaiďi waumini wamṭegemee Mungu ṭu k̇ a matatuzi ya matatizo yoṭʰe yanayowakabili hivo “kuvunja upanga” wa siyasa na kuweka imani k̇ a Ṁenyezi Mungu. Uṭafiṭi wetu una naṭija ya kuwafafanuliya wanaluǧa umuhimu wa nahau za kiSwahili katika fasihi na haswa ikiwa nahau hizo zina aťari za uhasi kama lilivo neno siyasa leo.

Description

Jarida la Kutumiya Alama za Kifasihi Kisiyasa ili Kušajiiša Mṭaji wa Kijamii: Kaďiya ya Sufi Ṁanalemba Kuvunja Upanga katika Uṭeṇḍi wa Siri Li Asrari

Citation

Karama, M., Muhia, A., wa Mutiso, K. & Chimerah, R. (2025). Kutumiya Alama za Kifasihi Kisiyasa ili Kušajiiša Mṭaji wa Kijamii: Kaďiya ya Sufi Ṁanalemba Kuvunja Upanga katika Uṭeṇḍi wa Siri Li Asrari. East African Journal of Swahili Studies, 8(1), 201-215. https://doi.org/10.37284/jammk.8.1.2760

Endorsement

Review

Supplemented By

Referenced By