Si t̪end̪i zot̪ʰe za kabla ya karne ya ishirini ni utambaji wa kingano nyengine ni ufunzaji: Kiyelelezo cha ut̪end̪i wa siri li asrari

Loading...
Thumbnail Image

Date

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

Jarida la Afrika mashariki la masomo ya Kiswahili

Abstract

Fikra iliyomo katika mawand̪a ya fasihi ya Kiswahili ni kuwa ut̪end̪i ni maelezo marefu ya mapisi ya jamii kiushairi. Makala haya yanat̪aka kuonesha kwamba si t̪end̪i zot̪ʰe zenye madhumuni haya. Kupitiya Ut̪end̪i wa Siri li Asrari tut̪aonesha kwamba mtʰunzi Mwanalemba alikuwa na niya t̪angu mwanzo ya kuweka d̪arasa kuhusu hirizi ya majina ya Mwenyezi Mungu. D̪arasa hii ameigawanya kama namna t̪aasisi za kielimu zinavopendekeza ienreshwe kiskuli na ameyat̪owa mawazo yake kit̪aalamu. Nadhariya ya Usemezano kupitiya dhana ya Unrimi imetusaidiya kuuwangaziya ut̪end̪i huu na tumefaidika na vigezo va: maudhui, ut̪euzi wa misamiat̪i na mitinro ya uwasilishaji, na mukt̪adha wa matʰumizi ya maneno hayo kama njiya ya kutambuwa aina ya lugha inayotʰumika. Kwa kwangaziya mitinro ya uwasilishaji katika d̪arasa ya hirizi tumepata kujuwa kwamba mtʰunzi alikuwa na dhamira ya kutufunza badala ya kutamba hadithi ya kingano.

Description

East African journal of Swahili studies

Citation

Karama, M., Chimerah, R., & Mutiso, K. (2021). Si T̪end̪i zot̪ʰe za Kabla ya Karne ya Ishirini ni Utambaji wa Kingano Nyengine ni Ufunzaji: Kiyelelezo cha Ut̪end̪i wa Siri li Asrari. Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 3(1), 51-57.

Endorsement

Review

Supplemented By

Referenced By